Uundaji wa maneno ni shughuli ya kuunganisha viambajengo (vipashio) mbalimbali ili kupata maneno tofauti yenye maana mbalimbali ambazo ni kamili.
Kwa kuwa maendeleo ya jamii hubadilika, hukua na kuongezeka hivyo hivyo lugha nayo hukua na kubadilika kwa lengo la kukidhi haja ya mawasiliano.
Ili msamiati uongezeke lazima maneno yaundwe kwa lengo la kuboresha mawasiliano kulingana na wakati uliopo.
Kupata msamiati wa kutosha katika lugha husika ili kukidhi mabadiliko yanayojitokeza.
Kukabiliana na suala la maendeleo ya sayansi na teknolojia katika ongezeko la maneno mapya.
Ubunifu wa maneno mbalimbali hutokana na njia mbalimbali kama vile uambishaji wa maneno, kubadili mpangilio wa herufi kutohoa maneno ya lugha nyingine, kuambatanisha maneno, kufananisha sauti, umbo, mlio.
1. Maana
Mfano; Baba, Mungu, Fikiri, bora
Katika Kiswahili, mofimu inaangaliwa katika daraja la vipashio vya lugha. kipashio hiki hakiwezi kuvunjwavunjwa zaidi bila kupoteza maana.
Mfano:
1. Mtoto (Watoto)
AINA ZA MOFIMU
Kuna aina kuu mbili za mofimu
Mofimu huru (sahihi)
Mofimu tegemezi
Ni mofimu inayoweza kusimama peke yake na kuweza kutumiwa katika tungo bila kuwa na kiambishi chochote. Mofimu huru zina hadhi ya neno na zinaweza kuwa aina yoyote ya neno kama vile: -
Majina (nomino): juma, simba, baba, mama, dada, kaka
Viwakilishi: mimi, sisi, yeye, wao, ninyi
Vivumishi: safi, chafu, kile, refu
Vitenzi: Sali, tafiti, jibu
Viunganishi: na, hata, hadi
Vielezi: haraka , polepole, sana, mno
Ni mofimu zinazofungamana na mofimu nyingine na zinapotumika hutegemeana ili kueleza dhana iliyokusudiwa. Mofimu hizi zinapofungamana huunda neno. Mofimu zinazounda neno huweza kuwa mbili au zaidi kulingana na mchangamano wa dhana ulio katika neno linaloundwa
Mfano:
Mtoto - m- toto
Watacheza - wa – ta – chez – a
Anasoma - a – na – som –a
Mkulima - m – ku – lim –a
Mfano:-
Neno “analima” lina mofimu nne (4) ambazo hufungamana na kujenga neno “analima” kila moja ya mofimu hizi isimamapo peke yake haina maana yoyote isipokuwa ina maana kisarufi ambayo humuwezesha mwanaisimu kuchambua maana ya mofimu hiyo.
Analima - a – na- lim – a
A – kiambishi awali kipatanishi cha nafsi ya III umoja
Na – kiambishi awali cha wakati uliopo
Lim – mzizi wa neno
A – kiambishi tamati
Dhima kuu ya mofimu ni kuongeza msamiati. Msamiati huo unaweza kuongezeka kwa kuunda neno zima. Pia msamiati unaweza kuundwa kwa shina moja kwa kuweza kuunda na kutoa maneno yenye maana mbalimbali.
Mfano:-
Neno “cheza” linaweza kuwa : mchezaji, mchezo, wanachezea, tulicheza, uchezeshaji, alimchezesha n.k.
Vilevile mofimu tegemezi zina dhima mbalimbali tofauti na uundaji wa msamiati. Baadhi ya dhima hizi ni kama vile,
kudokeza nafsi
kuonesha njeo (wakati)
kuonesha/ kudokeza urejeshi
kudokeza ukanushi
kudokeza kauli mbalimbali
(i) Maana
- Uambishaji ni kitendo cha kupachika kiambajengo (mofimu) cha neno kwenye mzizi wa neno ili kukamilisha muundo wa neno
AU
AU - Viambishi ni mofimu zinazowekwa kwenye mzizi wa neno na kukamilisha muundo wa neno.
Kwa mfano neno: ANAYEJIPIKIA
Viambishi awali (mwanzoni) vyake ni A – NA- YE – JI
Viambishi tamati ni –I – A – na mzizi wa neno hilo ni – PIK-
AINA ZA VIAMBISHI
- Hivi ni viambishi vinavyowekwa kabla ya mzizi wa neno navyo ni vitano
(ii) Viambishi ngeli Mfano:
M – tu = wa – tu
M – ti = mi – ti
M – zuri = wa – zuri
M – safi = wa – safi
Hivi hujitokeza katika vitenzi na wakati fulani huitwa viambishi awali vya nafsi
Mfano: - Umoja Wingi
Ni – nalima tu – nalima (nafsi 1)
U – nalima m – nalima (nafsi 2)
A – nalima wa – nalima ( nafsi 3)
Hivi huonesha wakati tendo limefanyika katika kitenzi
Mfano: analima
A – na- lima (wakati uliopo)
A – li – lima (wakati uliopita)
A – ta – lima (wakati ujao)
Hivi huonesha hali mbalimbali katika kitenzi
Mfano: -
Hu – lima (hali ya mazoea)
A – me – lima (hali timilifu)
A- nge – lima ( hali ya masharti)
Hivi hutaja mtenda wa jambo
Ni – na- ji – kata
A – na – ye – sema
U – li – o – enea
Hivi hutaja mtendwa wa jambo
Mfano: - Tuli – u – panda
Nina – i – soma
Ana – m – piga
Wana – ni – soma
Hivi huwekwa katika kitenzi ili kukamilisha hali ya kukanusha, viambishi vya kukanusha katika lugha ya Kiswahili ni ha – hu – na – si
Mfano: -
U – naimba hu – imbi
Ni – nacheza si – chezi
A – naimba ha- imbi
Ni viambishi vinavyopachikwa ndani ya mzizi wa neno na hivyo kuukuta katika sehemu mbili.
Viambishi kati havitokei katika Kiswahili lakini vipo katika sehemu nyingine, mfano kiebrania.
(c) Viambishi tamati
Hivi ni viambishi vinavyoambishwa baada ya mzizi wa neno navyo ni vya aina mbili.
Hivi hutokea baada ya mzizi wa kitenzi bila kubadilisha umbo la mzizi wenyewe. Viambishi tamati maana hutaja maana au dhana.
Mfano: -
Lim –a
Lim – wa
Chez – a
Chez – wa
Hivi ni viambishi vinavyoandikwa baada ya mzizi wa kitenzi viambishi tamati vijenzi navyo hutokea mara baada ya mzizi wa kitenzi na vina kazi kuu nne.
Kuleta maana ya ziada ya kule kwenye maana ya asili iliyobebwa na mzizi wa kitenzi.
Mfano: -
Lima – limia- limika – limisha – limiwa
Tendo – tendea – tendeka – tendesha – tendewa
Kujenga mzizi mpya wa kitenzi ambao utabebeshwa maana ya asili ya kitenzi na maana ya ziada. Mzizi huu mpya huitwa “mzizi wa mnyambuliko”
Mfano: -
(d) Huweza kubadili neno toka aina moja na kuingia aina nyingine
Mfano: -
Omba – ombeana – ombaji – ombeka – ombi – ombeaji
T T N T N T
(e) Kuweza kuzalisha kauli mbalimbali za tendo kama ifuatavyo;-
Kauli ya kutenda;- Chez – a Chek – a
Imb – a
Kauli ya kutendwa;- Chez – wa
Chek – wa
Imb – wa
Kauli ya kutendeka;- Chez – ek – a
Chek – ek – a
Imb – ik – a
Kauli ya kutendewa;- Chez – ew –a
Chek – ew – a Imb – iw – a
Kauli ya kutendea Chez –e –a
Chek – e – a
Imb –i –a
Kauli ya kutendeana Cheze – an – a
Cheke – an – a
Imbi – an – a
Kauli ya kutendesha Cheze – sh – a
Cheke – sh – a
Imbi – sh – a
Mzizi au kiini ni ile sehemu ya neno inayobakia baada ya kuondolewa aina zote za viambishi yaani viambishi awali na tamati (mzizi ni sehemu isiyobadilika).
Kuna aina mbili za mzizi
Huu ni mzizi unaobakia baada ya kuondolewa viambishi tamati vijenzi. Mzizi huu mpya hubeba maana ya ziada ya hivyo viambishi maana kama vile:
Lima lim-
Lewa lew- Cheza chez-
Ona on-
Huu ni aina ya mzizi ambao hujengwa na mzizi asilia pamoja na viambishi tamati vijenzi. Mzizi huu mpya hubeba maana ya ziada ya hivyo viambishi.
Tema tem Temana Teman
Pata Pat Patisha Patish
Lia Li Lilika Lilik
Kula Kul Liwa Liw
Soma Som Somana Soman
Shina la kitenzi ni mzizi wowote (yaani mzizi asilia au mzizi wa mnyambuliko) uliofunguliwa irabu -a- isiyo na maana maalum ya sarufi.
Mzizi shina
Lim + a lima
Chez + a cheza
Fik +a fika
Liw +a liwa
Vitenzi vyenye asili ya kigeni ambao huishia na irabu e, i, u katika mzizi asilia yao.
Mfano: -
Vitenzi hivyo, mzizi asilia na shina huwa kitu kimoja
Mzizi = shina + a
Shina = mzizi + a
KUBAINISHA MOFIMU AU VIAMBISHI
Kubainisha mofimu (viambishi) ni kitendo cha kutenga neno katika mofimu au viambishi vinavyolijenga.
HATUA MUHIMU KATIKA KUBAINISHA MOFIMU
Hatua zifuatazo ni muhimu katika kubainisha mofimu nazo ni: -
Kutambua aina ya neno ( neno huru au changamano) huundwa na mofimu tegemezi. Neno huru halivunjwivunjwi lakini neno changamano linavunjwavunjwa na kubainisha mofimu zake. Mfano wa neno huru = dada, kaka, mama.
Mfano wa neno changamano = a – na – on – a
= anaona
Kutenga (kuvunjavunja) mofimu au viambishi vinavyounda neno hilo yaani tambua viambishi awali, mzizi, kiini na viambishi tamati. Viambishi na mzizi hupatikana katika neno changamano
Mfano: -
Bainisha mofimu katika maneno yafuatayo na eleza kazi za kila mofimu.
Anasoma - a – na- som – a
1 2 3 4
Kiambishi awali kipatanishi nafsi III umoja
Kiambishi awali cha wakati uliopo
Mzizi wa kitenzi
Kiambishi tamati
Dunia - hili ni neno huru ambalo huundwa na mofimu hizi hazivunjwivunjwi
Waliompiga - wa – li- o – m – pig – a
1 2 3 4 5 6
Kiambishi awali kipatanishi nafsi ya tatu wingi
Kiambishi awali cha wakati uliopita
Kiambishi awali rejeshi cha watenda
Kiambishi awali rejeshi cha watendwa
Mzizi wa kitenzi
Kiambishi tamati
DHIMA YA MOFIMU/ VIAMBISHI
1. Kuonesha nafsi katika kitenzi
Mfano: -
Ni – nasoma= Tu – nasoma - I
U – nasoma = m – nasoma - II
A – nasoma = wa – nasoma- III
2. Kuonesha njeo katika vitenzi
Mfano: -
A – na – cheza - wakati uliopo
A – li – cheza - wakati uliopita
A – ta – cheza - wakati ujao
Kuonesha umoja na wingi katika nomino na viambishi
Mfano: - M – toto = wa – toto
Ki – su = vi -su
Kuonesha hali mbalimbali za kitenzi
Mfano: - hali ya masharti
A – ki – ja
A – nge – ku – ja
Mfano: - ni – nalima - si – limi
– nacheza - ha – chezi
U – naimba - hu – imbi
Kuonesha urejeshi wa mtenda au mtendwa katika kitenzi
Mfano: - A – na – ye – lima - Mtenda
– na – u – penda - mtendwa
Kuonesha kauli mbalimbali za vitenzi
Kauli ya kutenda - a – na – pik - a
Kauli ya kutendea - a – na -pik -i – a
Kauli ya kutendewa- a – na – pik – iw – a
Kauli ya kutendeana - wa – na – pik – ian – a
Kauli ya kutendesha - a – na – pik - ish – a
Kauli ya kutendwa - a – na – pik – w – a
TOFAUTI YA MOFIMU NA SILABI
Unyambulishaji unatokana na neno “nyambua” ikiwa na maana refusha au vuta kitu.
Mnyambuliko ni kitendo cha uvutaji au urefushaji kipashio / vipashio katika mzizi wa neno. Aidha mnyambuliko unahusu upachikaji wa mofimu zinazofuata mzizi wa neno. Mofimu hizi huitwa mofimu fuatishi (viambishi tamati)
Mfano:-
Soma - Som – e – a
Som – ek –a
Som – esh – a
Som – w – a
Som – ean – a
Vitenzi vyote vya Kiswahili isipokuwa kitenzi kishirikishi “ni” vinaweza kunyambulika.
Mfano: -
Piga – pigia, pigana, pigisha, pigwa, pigiana, cheza, chezea, chezeana, chezeshwa, chezwa.
Baadhi ya majina ya ujumla hupokea viambishi tamati na mengine hupokea viambishi tamati vijenzi.
Mfano: -
Nyumba - nyumbani
Bustani - bustanini
Hewa - hewani
Maji - majini
Hivi huchukua viambishi tamati maana
Mfano: -
Viwakilishi vya nafsi kama vile
Mimi - miye
Wewe - weye
Sisi - siye
Ninyi - niye
Viwakilishi virejeshi vya amba.
Hivi huchukua viambishi tamati vijenzi
Mfano: -
Safi - safisha, safishwa, safishia, safishika
Fupi - fupika, fupisha, fupishika, fupishwa
Refu - refusha, refushwa, refushika
Hesabu ndogo ya viunganishi huchukua viambishi tamati vitenzi.
Mfano : - Labda, labdatisha, labdilika, labdishwa.
DHIMA YA MNYAMBULIKO
Mnyambuliko wa maneno hukuza msamiati wa lugha husika.
Mnyambuliko wa maneno hupanua maana ya maneno.
Mnyambuliko wa maneno huzalisha kauli mbalimbali za vitenzi kutenda, kutendwa, kutendea, kutendeka, kutendana, kutendeana kutendesha, kutendeshwa.
0 Comments