๐‘ท๐’“๐’†๐’Ž๐’Š๐’–๐’Ž ๐‘ฝ๐’†๐’“๐’”๐’Š๐’๐’|๐‘ญ๐’–๐’๐’ ๐‘ท๐’๐’”๐’•๐’” ๐‘ผ๐’๐’๐’๐’„๐’Œ ๐‘ต๐’๐’˜

DEMO~PAPER 03-QNS

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SINGIDA MUNICIPAL COUNCIL 021 KISWAHILI

Time: 2:30 Hours JULAI 2023

MAELEKEZO:

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi (10)

  2. Jibu maswali yote

  3. Majibu yote yaandikwe kwenye nafasi ulizopewa

  4. Majibu yote yaandikwe kwa kalamu ya wino wa bluu au mweusi

  5. Vifaa vyote vya mawasiliano haviruhusiwi katika chumba cha mtihani.




SEHEMU A (ALAMA 15)

1. Jibu maswali yote katika sehemu hii.

i) Sauti za lugha ambazo hutamkwa bila kuwepo kwa kizuizi chochote kwenye mkondo kwa hujulikana kama:-

  1. sauti

  2. Herufi

  3. Irabu

  4. Konsonanti


ii) Silabi zinazotokea katikati au mwishoni mwa kila mstari wa shairi huitwaโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.

  1. Vina

  2. Mizani

  3. Sitiari

  4. Vituo


iii) Kiimbo hufasiliwaje katika mazungumzo?

  1. Kupanda na kushuka kwa mawimbi ya sauti

  2. kuzungumza na kuongea kwa sauti

  3. kuzungumza kwa kupandisha mawimbi ya sauti

  4. kuzungumza kwa kushusha mawimbi ya sauti


iv) Dhana ipi kati ya hizi zifuatazo haina maana Zaidi ya moja?

  1. Kaka amefua nguo

  2. Nipe sahani ya kulia

  3. Eva amenunua kanga

  4. John amempigia mpira


v) Mkisi ameenda Dodoma. Neno Dodoma limetumika kama

  1. Kihisishi

  2. Nomino

  3. Kiwakilishi

  4. Kielezi


vi) Mawazo makuu ya mtunzi wa kazi ya fasihi humfikia mlengwa kwa njia ipi kati ya hizi zifuatazo.

  1. Fani

  2. Falsafa

  3. Migogoro

  4. Dhamira


vii) Ipi ni tofauti ya msingi kati ya mashairi na ngonjera?

  1. Mpangilio wa vina na mizani

  2. Idadi ya mizani na mishororo

  3. Majibizano baina ya watu wawili au Zaidi

  4. Mpangilio wa silabi na lugha ya mkato.


viii) Bosi samahani kuna barua yako hapa โ€œMtindo huu wa mazungumzo unatumika wapiโ€?

  1. Ofisini

  2. Kiwandani

  3. Shambani

  4. Kanisani


ix) Sababu zifuatazo husababisha kutokea kwa utata katika tungo isipokuwa

  1. Neno kuwa na maana Zaidi ya moja

  2. Kuzingatia taratibu za uandishi

  3. Kutumia maneno yenye maana ya picha

  4. Kutotamka neno ulilokusudia kwa usahihi


x) Seti ipi ni sahihi kuhusu vipengele vya fani katika fasihi simulizi?

  1. Dhamira, migogoro, mtindo na mafunzo

  2. Ujumbe, matumizi ya lugha, wahusika, mtindo na muundo

  3. Wahusika, matumizi ya lugha, muundo, mtindo na mandhari

  4. Migogoro, Ujumbe,wahusika, mafunzo na mtindo

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.