๐‘ท๐’“๐’†๐’Ž๐’Š๐’–๐’Ž ๐‘ฝ๐’†๐’“๐’”๐’Š๐’๐’|๐‘ญ๐’–๐’๐’ ๐‘ท๐’๐’”๐’•๐’” ๐‘ผ๐’๐’๐’๐’„๐’Œ ๐‘ต๐’๐’˜

DEMO|PAPER 71-QNS

 

ST. MARYโ€™S MBEYA SECONDARY SCHOOL

MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA KWANZA KIDATO CHA TATU JULAI 2022 MSIMBO: 021 KISWAHILI

Muda: Saa 2:30

MAELEKEZO:

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).

  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali matatu (3) kutoka sehemu C.

  3. Sehemu A ina alama kumi na tano (15), sehemu B alama arobaini (40) na sehemu C ina alama arobaini na tano (45).




SEHEMU A (ALAMA 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya

jibu hilo kwenye kijitabu chako cha kujibia.

i.Neno โ€œChawaโ€ lenye maana ya mfuasi au kibaraka wa mtu fulani linaweza kuingizwa kwenye kundi gani la misimu kati ya haya?;

  1. Misimu ya pekee

  2. Misimu ya kihuni

  3. Misimu bandia

  4. Misimu ya kitarafa

  5. Misimu zagao


ii. โ€œMzee Mitomingi amelewa pombeโ€. Je, neno Mitomingi katika tungo hii limetumika kama aina gani ya kivumishi?

  1. Kivumishi cha pekee

  2. Kivumishi cha jina kwa jina

  3. Kivumishi cha sifa

  4. Kivumishi cha namna

  5. Kivumishi cha idadi


iii.Mwalimu wa Kiswahili alisikika akifundisha wanafunzi namna ya kufuatisha maneno katika sentensi ili kuleta maana sahihi.Kwa kuzingatia sarufi ya Kiswahili, je,mwalimu alikuwa anafundisha tawi lipi la sarufi kati ya haya?:

  1. Sarufi Matamshi

  2. Sarufi Muundo

  3. Sarufi Maana

  4. Sarufi Maumbo

  5. Sarufi Mofolojia


iv. Mzee Mwakipesile ana watoto watano, wanne kati ya hao wamebatizwa majina kutoka nomino za pekee na mmoja amebatizwa jina kutoka nomino za dhahania.Je, unafikiri mtoto wa mzee Mwakipesile ambaye ana jina kutoka nomino za dhahania atakuwa nani kati ya hawa?;

  1. Januari

  2. Faraja

  3. John

  4. Amosi

  5. Masanja


v.Mkuu wa shule wakati anawashauri wanafunzi waliofanya vibaya mtihani alisema kazeni kamba .Je,mkuu wa shule alitumia kipera gani cha semi kuwasihi wanafunzi wake kuongeza bidii?

  1. Nahau

  2. Methali

  3. Kitendawili

  4. Mizungu

  5. Msemo


vi. Mwajuma ni mvuvi mahiri katika ziwa Nyasa na hupenda kuimba nyimbo za kujiliwaza awapo katika shughuli zake za uvuvi.Je, nyimbo zinazoimbwa katika muktadha huu kifasihi huitwaje?

  1. Kimai

  2. Tendi

  3. Wawe

  4. Kongozi

  5. Nyiso


vii. Wakati wa sherehe za Mei mosi mwaka huu,wafanyakazi walishuhudia ushairi wa malumbano kuhusu ipi ni kazi muhimu kati ya udaktari na ualimu na mwishowe watambaji walikubaliana kuwa kazi zote ni muhimu kwa jamii. Je, unafikiri wafanyakazi walikuwa wanashuhudia kipera gani kati ya hivi?

  1. Maghani

  2. Majigambo

  3. Ngonjera

  4. Tenzi

  5. Tendi


viii. โ€œIli kamusi iweze kutumika katika utafiti wa chimbuko la lugha ni lazima iwe inafafanua asili za manenoโ€ Je,ni msamiati gani katika kamusi hutumika kumaanisha asili ya neno?

  1. Kisawe

  2. Vitawe

  3. Etimolojia

  4. Homonimu

  5. Kibadala


ix. Rukia alipoulizwa swali lililomtaka abainishe dhima tano za viambishi awali,alitoa hoja nne zilizo sahihi na hoja moja isiyosahihi.Ibaini hoja moja ya Rukia ambayo haikuwa sahihi miongoni mwa hizi;

  1. Kudokeza kauli mbalimbali

  2. Kudokeza njeo

  3. Kudokeza nafsi

  4. Kudokeza ukanushi

  5. Kudokeza urejeshi


x. Mhusika Sekai katika riwaya ya Takadini alikataa kuolewa na Manyamombe Kwa sababuโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ;

  1. Sekai hakumpenda Manyamombe

  2. Manyamombe alikuwa mzee mno

  3. Hakutaka kutenganishwa na Takadini

  4. Manyamombe alikuwa masikini

  5. Manyamombe alikuwa na wake wengi

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.