๐‘ท๐’“๐’†๐’Ž๐’Š๐’–๐’Ž ๐‘ฝ๐’†๐’“๐’”๐’Š๐’๐’|๐‘ญ๐’–๐’๐’ ๐‘ท๐’๐’”๐’•๐’” ๐‘ผ๐’๐’๐’๐’„๐’Œ ๐‘ต๐’๐’˜

๐ŸŒŠPAPER 14-Qns

MARKAZ ISLAMIC SEMINARY

JARIBIO LA MUHULA WA KWANZA KIDATO CHA TATU

KISWAHILI-021

Shape1

Aprili, 2024-Saa: 3:00

MAELEKEZO

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na moja(11).

  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na Bna maswali mawili (2) Kutoka sehemu C.

  3. Sehemu A ina alama kumi na sita (16), sehemu B alama hamsini nne(54) na sehemu C ina alama thelathini (30).

  4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na kila swali.

  5. Simu za mikononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.

  6. Andika Jina lako kamili katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia





SEHEMU A (Alama 16)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

  1. Katika kauli zifuatazo kauli ipi ina sifa tofauti na nyingine?

    1. Haraka haraka haina Baraka

    2. Aibu ya maiti aijuae mwoshwa

    3. Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu

    4. Amevaa miwani

    5. Mchelea mwana kulia yeye

  1. Sehemu ya lugha inavyoshughulikia maumbo katika sentensi

    1. Sarufi sintaksia

    2. Sarufi fonolojia

    3. Sarufi semantiki

    4. Sarufi mofolojia

    5. Sarufi Sentensi

  1. Mwalimu alipoingia darasani aliuliza “Nyote hamjafanya kazi yangu!. Kutokana na kauli aliyotoa mwalimu katika uzungumzaji mwalimu ametumia

    1. Kiimbo cha kuuliza

    2. Kiimbo cha mshangao

    3. Kiimbo cha masharti

    4. Kiimbo cha maelezo

    5. Kiimbo cha mshtuko

  1. “Kiatu kimepotea”. Sentensi hii inaweza kuwekwa katika kundi la ngeli ya ngapi

    1. Tatu

    2. Nne

    3. Tano

    4. Sita

    5. Saba

  1. Chagizo katika uchanganuzi wa sentensi hutumika katika mkabala wa

    1. Kimapokeo

    2. Kimuundo

    3. Kisiasa

    4. Kiupatanishi

    5. Kisintaksia

  1. Uchanganuzi wa sentensi katika mkabala wa kimuundo hujikita katika

    1. Kiima na kiarifu

    2. Kirai nomino na kirai kivumishi

    3. Kirai nomino na kirai kitenzi

    4. Kirai nomino na kishazi tegemezi

    5. Kirai kitenzi na kishazi tegemezi

  1. Nyuzi ulizoshonea zimekwisha. Viambishi vya O rejeshi katika sentensi ni

    1. U-Z0 katika ngeli ya tano

    2. O-ZO katika ngeli ya sita

    3. YO-ZO katika ngeli ya sita

    4. YO-ZO katika ngeli ya tano

    5. YO-ZO katika ngeli ya nne

  1. Zakia ni mwimbaji wa mashairi kila akiimba katika mshororo wa mwisho wa beti zake hufanana katika kila ubeti. Je tunaweza kuupa jina gani kati ya haya kishairi

  1. Kituo bahari

  2. Mshororo uradidi

  3. Mshororo takriri

  4. Kituo bahari

  5. Kituo

  1. Katika utumizi wa kazi za fasihi kuna jambo moja linalodhihirisha upekee wa mtunzi. Ni jambo gani hilo?

  1. Muundo wa kazi husika

  2. Mtindo wa kazi husika

  3. Wahusika wakazi husika

  4. Jina la mtunzi wa kazi husika

  5. Jina la kazi husika

  1. Zakia na Sumaiyyah walikubaliana kuwa “ Watamfulia mwalimu wao”. Je wazo hilo la Zakia na Sumaiya lipo katika kauli ipi katika ya hizi.

  1. Kutendea

  2. Kutendeana

  3. Kutendewa

  4. Kutendwa

  5. Kutendeka

2. Oanisha dhana za kifungu A ili kurandana na dhana iliyopo kifungu B

KIFUNGU A

KIFUNGU B

  1. Shamirisho

  2. Chagizo

  3. Ambatani

  4. Changamani

  5. Prediketa

  6. Sahili

  1. Ni sehemu ya sentensi inayokaliwa na kitenzi

  2. Ni aina ya sentensi iliyojengwa kwa sentensi mbili au zaidi kwa kutumia kiunganishi

  3. Ni aina ya sentensi inayokaliwa na vielezi ……

  4. Ni aina ya sentensi inayoundwa na kishazi huru kimoja

  5. Ni sehemu ya kielezi inayopatikana upande wa kiarifu

  6. Ni sehemu ya sentensi inayokaliwa na nomino dhahania

  7. Ni nomino inayopatikana upande wa kiarifu

  8. Ni aina ya sentensi inayoundwa kishazi tegemezi kimoja au zaidi

  9. Ni aina ya sentensi yenye muundo wa kirai na kiarifu

SEHEMU B (Alama 54)

3. Mwandishi huweza kumfinyanga mhusika kwa namna atakavyo. Thibitisha ukweli huu namna mwandishi wa riwaya ya Watoto wa Mama Ntilie alivyomfinyanga mhusika mwanaume. Kwa hoja Sita madhubuti



4.

  1. Sentensi hutungwa kwa kufuata Viambajengo maalumu ambavyo huweza kuleta maana kamili katika sentensi hiyo. Thibitisha usemi huu kwa kutunga sentensi kutokana na Vipashio vifuatavyo

  1. N + Ts + Ts + T

  2. W + V + T + E

  3. N + t + N + V

  4. H + T

  1. Kamusi ni kitabu chenye orodha ya maneno yanayopangwa kialfabeti na kutoa taarifa za lugha husika. Kutokana na kamusi zilizopo hapo chini eleza kundi la kamusi husika

  1. Baba (n) ni mzazi wa kiume

  2. Mama (n) ni mzazi wa kike, A female parent

  3. Baba (n) ni mzazi wa kiume, A male parent- mmale yamtzalile mwana.

  1. Sentensi huweza kuchanganuliwa kwa kutumia njia na mkabala maalum. Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya jedwali kwa mkabala wa kimuundo

Mbuzi aliyenunuliwa jana amechinjwa leo asubuhi

  1. Kwa mifano madhubuti onesha muundo wa kirai nomino. Hoja sita



  1. Katika utanzu wa semi katika kipera cha methali huwa zipo zenye kurandana. Thibitisha ukweli huu katika methali zifuatazo kwa kuandika methali inayorandana katika semi zilizopo hapo chini

    1. Mimi nyumba ya udongo sihimili kishindo

    2. Miruzi mingi humpoteza mbwa

    3. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti

    4. Usipoziba ufa utajenga ukuta

    5. Subira yavuta heri

    6. Uvivu nyumba ya njaa

8.

  1. Mke wa kwanza Maduo, huyu ninamtukuza

Ni mponda kwa ukoo, Asili yake Homboza

Ametuletea koo, Jinale ni maangaza Amuoe mke gani, kaka Chebi jamani?

  1. Na sasa anae Jina, mzuri tena kijana

Kutwa wakiongozana, mithili mapacha wana

Hata enzi ya korona, mikono walishikana

Amuoe mke gani, Kaka chebi jamani

MASWALI:

    1. Kichwa cha shairi kinachofaa

    2. Elezea mtindo uliotumika katika uundaji shairi hili na namna alivyoichezea lugha katika matumizi yake

    3. Eleza kwa kutaja migogoro iliyojitokeza na suluhisho la mgogoro huo

SEHEMU C (Alama 30)

Jibu maswali mawili kutoka sehemu hii. swali la tisa (9) ni la lazima

  1. Waandishi huweza kutumia mandhari na kuibua dhamira katika kazi zao. Thibitisha kauli hii namna mwandishi wa riwaya ya watoto wa Mama Ntilie alivyoweza kutumia mandhari katika kuibua dhamira. Hoja sita madhubuti

  2. Miviga katika jamii ina hasara na faida zake. Dhihirisha usemi huu kwa kuelezea hasara za miviga kwa jamii. Tumia hoja sita madhubuti

  1. Methali huweza kuelimisha na kukosoa jamii. Thibitisha usemi huu kwa kutoa methali tatu zinazoelimisha na methali tatu zinazokosoa. Huku ukielezea mafunzo hayo na ukosoaji wake.

Shape2

→Get a Copy ←

Cookie Consent
We serve cookies on this site to analyze traffic, remember your preferences, and optimize your experience.
Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.
Site is Blocked
Sorry! This site is not available in your country.